Mama Kama Wewe Hakuna (Mother, their’s none like you!)

Mwana hutazama kisogo cha nina, wasemao walisemaYamkini maneno yamekataa kuitika, sijui ntasemajeMilizamu ya machozi yanitoka, nikikumbuka uliyopitiaFadhila na heshima mpe mama, Mola ‘takubariki Kaniweka utumboni mwako, nafasi ya kuona mwanga kanipaKanilea tangu utotoni, elimu ya mama ukanipaSkulini ulinituma nilipokomaa, stashahada na shahada n’taletaFadhila na heshima mpe mama, Mola ‘takubariki Mengi ulipitia, hivi nani wa kulinganishwa … Continue reading Mama Kama Wewe Hakuna (Mother, their’s none like you!)

Natamani Kukuona Tena (I long to see you again).

Nina uchungu moyoni, sikomi kutesekaKamwe sitaki kukumbuka, nasema sitakiLimekuwa ni donda, lakataa kuwa kovuNani kasema baada ya dhiki ni faraja? Pengo kubwa uliacha, kuzibwa haliweziKaniacha nifilie mbali, mimi kiumbe dhaifuChakula hakiliki, kimekuwa kichunguNani kasema baada ya dhiki ni faraja? Nilikuenzi ja mboni ya jicho, mama ajuaNikakupumbaza kwa huba, baba ni shahidiMapenzi yasojua kufa, kawaulize wanakijijiNani … Continue reading Natamani Kukuona Tena (I long to see you again).

Nitaandika Siku Moja (I’ll write one day).

Kwa hakika siamini, siamini ninayoyawazaNimeshindwa kufasiri , ni kama kiumbe dhaifuUbongoni hakukaliki, mawazo chungu nzimaSijui nifanyeje, ila natabasamu Nina ndoto, ila si ndoto ya AmerikaNdoto ya ajabu, ndoto ndani ya ndotoLabda ni ndoto ya kitoto, yakosa mashikoNashangaa nitakuelezaje nina ndoto? Nitaandika siku moja, mpaka nimalize winoNitaandika siku moja, maneno yanitokeNitaandika siku moja, shuleni vitabu wavisomeNitaandika … Continue reading Nitaandika Siku Moja (I’ll write one day).